Msanii wa muziki wa Bongo Flava, Enock Bella aliyekuwa member wa
kundi la Yamoto Band amefunguka taarifa zinazodai amefunga ndoa.
Muimbaji huyo akizungumza na BEST DJ'S EVER TZ amesema si kweli amefunga ndoa
kama inavyozungumzwa na picha kuonekana ila itakafika wakati
atazungumza.
“Kwa sasa hivi nitadanganya siwezi kuzungumzia hilo suala, kuna
wakati nitazungumzia tu ila kuna vitu fulani naviweka sawa. Hapana
siwezi kusema nimefunga ndoa au sijafunga ndoa” amesema Enock Bella.
Japo wasanii wenzake aliokuwa nao Yamoto Band, yaani Aslay, Beka
Flavor na Maromboso walionekana kumpongeza Bella kupitia mitandao ya
kijamii kwa kuashiria amefunga ndoa.
BY MPIKO JUNIOR
No comments:
Post a Comment