Friday, December 29, 2017
Thursday, December 28, 2017
Wednesday, December 27, 2017
NEWS:LULU DIVA ATANGAZA KOLABO YAKE NA WIZKID
Msanii wa muziki Bongo, Lulu Diva afunguka ujio wa kolabo yake na Wizkid kutoka Nigeria.Muimbaji huyo wa ngoma ‘Give It To Me’ ameiambia The Playlist kuwa mwakani kuna uwekano wa kufanyika kolabo hiyo.
“Watengemee kolabo may be Wizkid, alikuwa rafiki yangu lakini tulikuwa tunachati na kukutana naye nafikri nakumbuka ile party Diamond alifanya Mwanza Wizkid alikuja ku-perform hapo ndio nilionana naye kwa mara kwanza” amesema Lulu Diva.
Ameongeza kuwa kwa upande wa Bongo wapo wasanii wengi ambao anawafikiria lakini kwa sasa anatamani kuja kufanya kolabo na Vanessa Mdee.
Monday, December 25, 2017
Saturday, December 23, 2017
Thursday, December 21, 2017
Wednesday, December 20, 2017
NEWS:Baraka The Prince azidi kulia mchezo mchafu YouTube
Msanii wa muziki Bongo, Barakah The Prince amedai kuwa bado video zake zinafanyiwa hujuma katika mtandao wa YouTube.
“Hiyo ishu ilianzia kwenye video yangu ya Sometimes views hawapandi, subscriber wanasimama, likes wanashuka, dislike wanakuwa ni wengi, wimbo unafanya vizuri mtaani halafu dislike zinakuwa ni nyingi, kwa hiyo kuna mchezo nilikuwa nafanyiwa ambao ni the same kwenye Nipe Nguvu,” amesema Barakah.
“Na promotion yote ninayokuwa naifanya kwenye mitandao ya kijamii views wanakuwa hawapandi, kuna wasanii ambao ni underground ambao sidhani kama wana mashabiki kama vile ninao mimi tumetoa video pamoja lakini views zao zinapanda kitu ambacho si cha kawaida,” ameongeza.
Tuesday, December 19, 2017
Monday, December 18, 2017
Thursday, December 14, 2017
Wednesday, December 13, 2017
Tuesday, December 12, 2017
Monday, December 11, 2017
Sunday, December 10, 2017
NEWS:NAVY KENZO WAPATA MTOTO
Wasanii Nahreel na Aika wanaounda kundi la Navy Kenzo ambao pia ni wapenzi wamejaliwa kupata mtoto wao wa kwanza hapo jana siku ya uhuru tarehe 9 disemba.
Kupitia kurasa zao za mtandao wa Instagram wameeleza furaha yao mara baada ya kupata mtoto huyu. Nahreel ameandika; #Gold z Finaly Here, God z good all the time #HappyIndependenceDayTz
Huku Aika naye akiandika; Mr Gold welcome to the world. Thank you God, and thank you all for ur prayers. #AlsoHappyBirthdayMum#HappyIndependeceDayTanzania
Saturday, December 9, 2017
NEWS:DIAMOND MATATANI TENA KWA KAULI ZAKE CHAFU DHIDI YA WANAWAKE
Msanii Diamond Platnumz anayetamba na Ngoma ya Sikomi ameingia matatani baada ya watu mbalimbali kumtuhumu kuwadhalilisha wanawake kupitia ujumbe wake aliouandika katika ukurasa wake wa Instagram.
Ujumbe huo ambao ulikuwa ni maalum kwa ajili ya kumtakia heri ya kuzaliwa mtoto wake wa kiume, Nillan, ulimtaka mtoto huyo akue salama ili aje awatumie wanawake vyovyote atakavyo kwa sababu anajituma ili amwandalie pesa ya kutumia vyovyote atakavyo atakapokuwa mkubwa.
“Nasemaje! Kua Uje kuwatembezea Baba… We swala la Kutafta ela niachie mie… Jukumu lako ni moja tu, Kupita nao…..Happy 1st Year Lanny!!!” Unasomekla ujumbe huo wa Diamond.
Friday, December 8, 2017
Thursday, December 7, 2017
Subscribe to:
Posts (Atom)