Saturday, December 9, 2017
NEWS:DIAMOND MATATANI TENA KWA KAULI ZAKE CHAFU DHIDI YA WANAWAKE
Msanii Diamond Platnumz anayetamba na Ngoma ya Sikomi ameingia matatani baada ya watu mbalimbali kumtuhumu kuwadhalilisha wanawake kupitia ujumbe wake aliouandika katika ukurasa wake wa Instagram.
Ujumbe huo ambao ulikuwa ni maalum kwa ajili ya kumtakia heri ya kuzaliwa mtoto wake wa kiume, Nillan, ulimtaka mtoto huyo akue salama ili aje awatumie wanawake vyovyote atakavyo kwa sababu anajituma ili amwandalie pesa ya kutumia vyovyote atakavyo atakapokuwa mkubwa.
“Nasemaje! Kua Uje kuwatembezea Baba… We swala la Kutafta ela niachie mie… Jukumu lako ni moja tu, Kupita nao…..Happy 1st Year Lanny!!!” Unasomekla ujumbe huo wa Diamond.
Friday, December 8, 2017
Thursday, December 7, 2017
NEWS:MR NICE AMKANA YOUNG DEE
Msanii mkongwe wa muziki wa bongo fleva kwenye miondoko ya TAKEU, Mr. Nice, amesema hamjui msanii Young D ambaye ametumia wimbo wake, na kwamba hakubaliani na kitendo cha yeye kutumia kazi yake.
Akizungumza na mwandishi wa East Africa Television,Mr. Nice amesema licha ya kutoruhusu mtu yeyote kutumia kazi zake, hajapata taarifa kutoka kwa Young D wala uongozi wake, na hajawahi kumjua kwenye maisha yake.
“Sijawahi kuongea wala kuruhusu binadamu yoyote kutumia kazi yangu yoyote bila makubaliano na ridhaa yangu mwenyewe iwe ni kwa kuniheshimu ama kunidhihaki, so far simjui huyo Young D at all , ndo namsikia kwako”, amesema Mr. Nice.
Kwa upande wa Young D amesema suala hilo tayari uongozi wake unalishughulikia ili kumalizana na malalamiko ya Mr. Nice, hata hivyo aliamua kufanya kama kumpa heshima kutokana na kukubali kazi zake alizokuwa akizifanya.
Wednesday, December 6, 2017
Tuesday, December 5, 2017
Sunday, December 3, 2017
NEWS:MANGE KIMAMBI AIBUA MAPYA SAKATA LA WEMA SEPETU KURUDI CCM
Mwanadada Mange Kimambi ameibukia sakata la Wema Sepetu kurudi CCM,ikiwa ni siku kadhaa zimepita tangu atabiri mpango wa Wema Kurudi CCM.
Akizungumza kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii Kimambi amesema Wema hajawaangusha watanzania pekee bali amejiangusha yeye mwenyewe kwa kutokua na msimamo.
“Hujawaangusha waTZ tu, umejiangusha mwenyewe pia, your fans and everyone who cared for you. Hivi kizazi hiki kina Winnie Mandela hakuna kabisa eehe? Nakuonea huruma mnoooo sababu umepoteza credibly yooooote kwenye jamii”Ameandikia Mange Kimambi.
Hivi karibuni Mange alisema kuwa anazo taarifa za uhakika kuwa Wema Sepetu pamoja na Mama yake watarudi chama cha Mapinduzi akidai kuwa mama yake amekubali kurudi isipokuwa anasuburiwa yeye.
Mange alisema mpango wa kurudi CCM unafuatia Wema na Mama yake kubanwa katika mambo mbalimbali kutokana na kuwa upande wa upinzani.
Wakati akitangaza kurudi CCM jana Wema alisema..
“Siwezi Kuendelea kuishi kwenye nyumba inayo nikosesha amani… Peace of mind is everything for me. Natangaza rasmi kuondoka Chadema na kurudi nyumbani” . Wema Sepetu.
Wema alijiunga chama cha Chadema mwezi februari mwaka huu akitokea chama cha Mapinduzi.
Subscribe to:
Posts (Atom)