Saturday, January 13, 2018
NEWS | MZEE YUSUPH AENDELEA KUOMBA WENYE NYIMBO ZAKE WAZIFUTE KWENYE SIMU ZAO
Aliyekuwa mwimbaji na Mkurugenzi wa bendi ya Jahazi Modern Taarab, Mzee Yusuf amefunguka na kutilia mkazo na kuwaomba watu hususani wanawake ambao bado wana nyimbo zake za Taarab kwenye simu wazifute ili iwe kheri zaidi kwenye imani yake na dini yak.
Mzee Yusuf alisema hayo alipokwenda Babati mkoani Manyara katika harakati ya kuzidi kukutana na watu na kuwaomba wazifute nyimbo zake hizo za Taarab kwa kuwa anaamini zinakwenda kinyume na imani yake.
“Niko Babati kuzidi kuwaomba Waislam wanifanyie ‘Ihsaan’ ya kuzidi kuniombea dua na kuzifuta nyimbo zangu kwenye simu zao kwa ajili ya dini ya ‘Allah’ iwe kheri na salama. Wengine nyinyi mpaka sasa simu zenu bado zinabalaa naombeni mzifute kwa ajili ya ‘Allah’ naona haya simu zikipigwa zikaita hizo nyimbo kwani najisikia vibaya sijui nifanyaje” alisema Mzee Yusuf
Aidha Mzee Yusuf alisema kuwa kwa sasa anaogopa na kuwataka wale ambao wanasema wamemkumbuka kwenye masuala ya uimbaji wa nyimbo za Taarabu waache kumkumbuka kwenye mambo hayo bali wamsaidie kwa kuzifuta nyimbo hizo. Mbali na hilo Mzee amewaomba watu wa vyombo vya habari na kwenye mitandao ya kijamii kufuta kazi zake zote hizo kwa ajili ya hisani ya ‘Allah’
NEWS | JOH MAKINI AFUNGUKA KUHUSU KOLABO YAKE NA FID Q
Kama wewe ni mpenzi au mdau wa muziki wa Hip Hop hapa Bongo, basi hakuna ubishi kuwa kolabo kubwa inayosubiriwa na mashabiki ni kolabo kati ya Joh Makini na Fid Q.
Je, unajiuliza kolabo hii huenda ikatokea? ukweli ni kwamba ondoa shaka kwa hilo kwani Joh Makini amesema kuwa ni muda tu unasubiriwa kwani wawili hao hawajahi kukaa pamoja kuzungumzia ishu za kolabo lakini endapo ikitokea nafasi ya kufanya hivyo watafanya.
“Mimi na Fid Q hatuna matatizo kama ambavyo watu wanafikiri, kwa sababu mimi mwenyewe binafsi sijawahi kuwa na matatizo naye na wala sijawahi kuona kama anamatatizo na mimi. Kwa hiyo mimi kama msanii na yeye kama msanii Chochote kinaweza kutokea anytime,“amesema Joh Makini kwenye kipindi cha Playlist cha Times FM huku akielezea kikwazo cha muda
“Ni vile labda hatujawahi kukutana kwenye hiyo vibe, hatujawa bado kwenye hiyo Chemistry ya kusema tufanye ngoma pamoja so you never know..hakuna mipaka 2018,“amemaliza Joh Makini.
Friday, January 12, 2018
Wednesday, January 10, 2018
Tuesday, January 9, 2018
Monday, January 8, 2018
Subscribe to:
Posts (Atom)