Sunday, November 5, 2017

NEWS:HUYU NDO DJ WA AFRIKA KUSINI ALIYEPIGIWA SIMU NA RIHANNA ILI WAFANYE COLLABO

Dj maarufu Africa na dunia nzima kutoka Afrika Kusini Dj Black Coffee amethibitisha kuwa kambi ya Rihanna imetaka afanye naye kazi.
Dj Black Coffee amethibitisha kufanya kazi na Rihanna nakusema tayari ameshatuma nyimbo kadha na kambi ya Rihanna imechagua mmoja ambayo wameipenda na Kazi imeshaanza
Dj Black Coffee ameendelea kusema kabla JAY-Z hajatoa album yake ya 4.44 alitaka kufanya naye kazi, Dj Black Coffee anasema “Swizz Beatz alinicheki kuhusu JAY-Z kutaka nifanye naye wimbo,Sababu ya Shauku kubwa nilishindwa kufanya wimbo huo, sikulala usiku kucha, nadhani Sikuwa tayari kwaajili ya kufanya wimbo na JAY-Z”
Dj Black Coffee anasema Ukiachana na Cassie, Riri na JAY-Z, Wasanii wengine wanaotaka kufanya kazi na mimi ni pamoja na Usher Raymond, Akon na Diddy.
    

No comments:

Post a Comment